Mwanamuziki Muhidin Maalim Gurumo ( kulia ) akiwa na mwanamuziki mwenzake Said Mabera
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Jakaya Mrisho Kikwete akimvisha nishani Muhidin Maalim Gurumo kuenzi mchango wake mkubwa katika muziki wa dansi nchini
Mwanamuziki Muhudin Maalim Gurumo aliyefariki dunia jana katika hospital ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam atazikwa kesho jumanne badala ya leo kama ilivyokuwa imetangazwa hapo awali kijijini kwao Masaki wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani.
Gurumo amefariki akiwa na umri wa miaka 73 hadi anastaafu muziki alikuwa na bendi ya Msondo Ngoma Music Band " Baba ya Muziki '. Pia alipata kuimba katika bendi za Sikinde, Orchestra Safari Sound " OSS "
Kabla ya kupelekwa kijijini Masaki kwa mazishi, Gurumo "Kamanda" kama alivyoitwa na mashabiki wake kwanza ataagwa nyumbani kwake Mabibo External.
Meneja wa Msondo Ngoma, Kibiriti amesema huu ni msiba mkubwa si tu kwa familia ya Maalim Gurumo, bali ni msiba kwa taifa zima kutokana na tungo mbalimbali alizopata kutunga Gurumo zenye kuelimisha jamii.
Amesema awali ilikuwa maziko yafanyike leo, lakini sasa yatafanyika kesho jumanne japo hakufafanunua zaidi.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni