.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 14 Aprili 2014

MWENDESHA MASHTAKA AMTUHUMU OSCAR PISTORIUS KWA KULIA LIA ILI KUTAKA AONEWE HURUMA

Mwendesha mashtaka katika kesi ya mauaji inayomkabili Oscar Pistorius ametoa pendekezo kuwa mwanariadha huyo wa Afrika Kusini anatumia ushawishi wa kuonyesha hisia kama kigezo cha kujinasua.

Pistorius aliangua kilio mara nne hii leo na pia alitapika mahakamani, jambo ambalo mwendesha mashtaka anahisi ni ujanja wa kutaka kuonewa huruma na watu.

Mwendesha mashtaka Gerrie Nel amesema Pistorius anaanza kujaribu kutumia mchezo wa hisia ambao hata hivyo hautamsaidia.
Pistorius alikiri kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp Februari mwaka 2013 kwa kumpiga risasi baada ya kudhani ni mtu aliyevamia nyumba yake. 

Picha juu inaonyesha risasi nne ambazo zilipenya katika mlango wakati mwanariadha huyo alipofyatua na kumuua mpenzi wake

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni