.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 13 Aprili 2014

UKRAINE KUWANG'OA WANAHARAKATI WANAOIUNGA MKONO URUSI WANAOSHIKILIA JENGO LA POLISI

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ukraine amesema vikosi vya nchi hiyo vimeanzisha operesheni ya kuwadhibiti wanaharakati wanayoiunga mkono Urusi wanaoshikilia kituo cha polisi tangu siku ya jumamosi.

Waziri huyo Arsen Avakov ametangaza kwenye ukurasa wake wa Facebook kuwa vikosi vyote vya ulinzi vinahusika katika zoezi hilo aliloliita la kukabiliana na magaidi, Mashariki mwa Mji wa Sloviansk.

Urusi imeonya kuwa matumizi yoyote ya nguvu dhidi ya wanaharakati Mashariki mwa Ukraine yataathiri mazungumzo ya mgogoro huo yanayotarajiwa kufanyika baadae wiki hii.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni