.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 25 Aprili 2014

WATU 22 WALAZWA HOSPITAL HUKO UGANDA BAADA YA KULA CHAKULA CHENYE SUMU BAADA YA MISA

Watu 22 wamelazwa katika hospitali ya Mkoa ya Mbarara nchini Uganda baada ya kudaiwa kula chakula chenye sumu siku ya jumapili ya Pasaka katika Kanisa la Mbarara. 

Wahubiri wa Kanisa hilo la Miracle Centre Church wakiwemo watoto na wahudumu wa Kanisa hilo lililopo eneo la Lugazi, walianza kulalamika maumivu makali ya tumbo baada ya kula wali, chapati, matoke, maharage na nyama baada ya misa kanisani hapo. 

Muhubiri wa Kanisa hilo, Douglas Kabuye akizungumza akiwa kalazwa hospitalini hapo, alisema chakula hicho kiliandaliwa mapema asubuhi kabla ya misa kisha kikaachwa jikoni kabla ya kuliwa baada ya misa. 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni