Chama tawala cha African National Congress ( ANC ) cha nchini Afrika Kusini mpaka sasa kinaongoza katika uchaguzi mkuu unaofanyika nchini humo.
Mpaka kufikia sasa, ANC inaonyesha kuwa baada ya kuhesabiwa kwa zaidi ya asilimia 25 ya kura zilizopigwa, chama hicho kinaongoza kwa asilimia 57.3 ya kura zote, kikifuatiwa na chama cha Democratic Alliance ambacho kimepata asilimia 29.2 ya kura zote zilizohesabiwa mpaka sasa.
Chama cha ANC kinaimani kubwa ya kushinda na kuendelea kuongoza Taifa hilo kwa muhula mwingine chini ya Rais wa sasa Jacob Zuma.
Watu milioni 25 wamejiandikisha kupiga kura nchini humo, katika uchaguzi ambao kuna jumla ya vituo 22, 000 vya kupigia kura nchi nzima.



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni