Zanetti akifuta machozi huku akibembelezwa na wachezaji
Mchezaji Javier Zanetti amecheza mchezo
wake wa mwisho katika dimba la San Siro akiwa Inter Milan, mchezo
ambao wameibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Lazio hapo jana.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 40,
ambaye aliichezea Inter Milani michezo 863 aliingia dimbani mnamo
dakika 52, akichukua nafasi ya beki wa kulia wa Brazil Jonathan na
kushangiliwa mno na mashabiki..
Siku ya Ijumaa, mchezaji huyo raia wa
Italia, alitangaza uamuzi wa kujiuzulu kusakata soka baada ya
kufanikiwa kutwaa makombe 19 na Inter Milan, ambapo sasa atakuwa
Mkurugenzi wa Klabu hiyo.
Zanetti akirushwa juu na wachezaji wenzake
Zanetti na familia yake wakiaga mashabiki
Shabiki wa Inter Milan akiangua kilio wakati wa kuagwa kwa Zanetti




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni