Ndege ikiwa na abiria 185 imelazimika
kugeuza angani wakati ikikatiza bahari ya Atlantic baada ya
wafanyakazi wake tisa kuanza kujisikia vibaya na kupata kizunguzungu,
wakiugua ugonjwa wa kutiririkwa na machozi.
Rubani wa ndege hiyo ya Shirika la
Ndege la Marekani aina ya A330 Airbus alimtaarifu tatizo hilo
muongozaji ndege wa uwanja wa Shannon wa Ireland, wakati ndege hiyo
ikipaswa kutua Dublin.
Ndege hiyo ilitua salama katika uwanja
huo na kuelekezwa kusima eneo la kando la uwanja huo ambapo abiria na
wafanyakazi wa ndege hiyo walishushwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni