.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 5 Mei 2014

KESI YA MWANARIADHA OSCAR PISTORIUS KUENDELEA KUNGURUMA LEO JIJINI PRETORIA

Kesi ya mauaji inayomkabili mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius inatarajia kuendelea leo baada ya mapumziko ya wiki mbili kwa upande wa mshitakiwa kuwasilisha utetezi wake.

Wataalam zaidi wataitwa wakati mwanasheria wa Pistorius akijaribu kupangua hoja za mwanasheria wa serikali kuwa mwanariadha huyo alimuua kwa makusudi mpenzi wake Reeva Steenkamp.

Pistorius amekuwa akikanusha kumuua kwa makusudi Reeva Steenkamp siku ya Valentine mwaka jana kwa kumpiga risasi akiwa amejifungia msalani.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni