.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 14 Mei 2014

MAKAMPUNI YAGOMBEA NYIMBO ZAIDI YA 13 ZA MAREHEMU BOB MARLEY

Mahakama Kuu ya London imeanza kusikiliza malumbano ya mgogoro wa hati miliki ya nyimbo zaidi ya 13 za mwanamuziki wa Jamaica Marehemu Bob Marley.

Wachapisha nakala za muziki Cayman Music wanajaribu kupata haki ya nyimbo hizo, miongoni mwao ikiwemo ya traki ya 'No Woman, No Cry'.

Kampuni hiyo imedai kuwa hawakuhusishwa wakati zikiuzwa haki za nyimbo hizo mwaka 1992 kwa Blue Mountain Music, na wakati Bob Marley akitia saini na watu wengine. Hata hivyo Kampuni ya Blue Mountain imesema nyimbo hizo zilihamishiwa kwao kwa mujibu wa makubaliano yao.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni