.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 14 Mei 2014

POLISI NCHINI BRAZIL YAWATAKA WATU WATAKAOIBIWA WAKATI WA KOMBE LA DUNIA KUWA WAPOLE

Polisi nchini Brazil wamewataka watalii nchini humo kuto piga kelele au kufanya jambo lolote lakujihami wakati watakapokumbana na tukio la shambulizi au uvamizi wa majambazi wakati wote watakapokuwa nchini humo.

Hiyo ni moja ya dondoo ambazo Polisi nchini Brazil wameandika kwenye kabrasha maalum kwa ajili ya kuwakumbusha wataliii nchini humo jinsi gani wanaweza kuishi salama wakati wa pilika pilika za michuano ya kombe la dunia.

Dhumuni hasa la dondoo hii, ni kutowafanya majambazi au wanyang'anyi kufanya maafa zaidi kwa mwathirika wa uhalifu, kwani kupiga kelele au kujaribu kujiokoa kunaweza kusababisha maafa zaidi.

Wachambuzi wa mambo wamehoji iwapo dondoo hizi zinampa mhalifu mwanya zaidi wa kufanya uhalifu. Hata hivyo Polisi hao wa Sao Paolo wamesema ni bora kuvamiwa na kuibiwa kuliko kuuwawa. Watalii wametakiwa kutokubeba vitu vya thamani hasa maeneo ya wazi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni