.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 5 Mei 2014

MAKAMU WA RAIS KENYA ASEMA MATUKIO YA UGAIDI HAYAWATISHI NA HAWATAONDOA MAJESHI YAO SOMALIA

Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto amesema kamwe serikali ya nchi hiyo haitatishwa na vitendo vya kigaidi vinayotokea sasa, na Kenya haitaondoa wanajeshi wake waliopo nchini Somalia kusimamia amani. 

Ruto ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja tu baada ya kutokea milipuko ya mabomu katika mabasi mawili ya abiria na kusababisha vifo vya watu 3 na wengine 86 kujeruhiwa jana jioni jijini Nairobi. 

Makamu huyo wa Rais wa Kenya amesema katu hawataondoa majeshi yao Somalia hadi nchi hiyo itakpokuwa salama.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni