Kampeni ya kutaka wasichana wa shule zaidi ya 200 waliotekwa wakiwa shuleni nchini Nigeria waachiliwe huru imezidi kushika kasi, baada ya mwanaharakati maarufu kijana nchini Pakistani, Malala Yousafzai ( pichani ) kujitokeza hadharani na kuomba nchi zote duniani kulaani kitendo hicho kilichofanywa na kundi la Boko Haramu katika jimbo la Borno, nchini Nigeria.
Malala binti aliyejipatia umaarufu baada ya kutekwa na wapiganaji wa Taliban na kupigwa risasi ya kichwa na kunusurika kifo, amesema kitendo cha wasichana hao kutekwa hakikubaliki na hakivumiliki.
Mke wa Rais wa Marekani Barack Obama, Michelle Obama akiwa ameshika bango lenye ujumbe wa wa kutaka kuachiliwa huru kwa wasichana hao
Tayari viongozi wa sehemu mbalimbali duniani wameanza jitihada za kuwatafuta na kuwaokoa wasichana hao, ambapo Rais Barack Obama ametangaza kupelekwa Nigeria kwa kikosi maalum cha wataalam ili kusaidia kuwatafuta na kuwaokoa wasichana hao.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni