Monica Lewinsky ameamua
kufichua mambo zaidi kuhusiana na kashfa ya uhusiano wake na
aliyekuwa rais wa Marekani ambapo amebainisha kuwa alikataa kitita
cha dola milioni 10, kutokana na kuona si jambo sahihi kupokea fedha
hizo.
Lewinsky aliyekuwa kimada
wa Bill Clinton, pia amelieleza jarida la Vanity Fair namna
alivyokuwa akikabiliana na mawazo ya kujiua mara baada ya kuibuka kwa
kashfa hiyo nzito iliyolitikisa taifa la Marekani mnamo mwaka 1998.
Monica Lewinsky, amekiri
kuwa ni kweli rais alitumia ubosi wake kuweza kumnasa lakini hata
hivyo uhusiano wao ulikuwa wa maridhiano ya pande mbili, na kwamba
alidai kudhalilishwa pale alipotolewa kafara kwa ajili ya kumlinda
Clinton wakati wa kampeni.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni