.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 12 Mei 2014

MTAALAM WA MAGONJWA YA AKILI ADAI PISTORIUS ANATATIZO LA KUJAWA NA HOFU YA MATUKIO YA UHALIFU

Mtaalam wa magonjwa ya akili ameieleza mahakama kuwa mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius anatatizo la kujawa na hofu ya matukio ya uhalifu wa kutumia nguvu tangu alipokuwa mtoto.

Meryl Vorster amesema kuwa vitendo vyake vilivyopelekea kumpiga risasi mpenzi wake Reeva Steenkam siku ya wapendano vilitokana na hali hiyo ya hofu ya uhalifu.

Mwendesha mashtaka sasa ametaka mwanariadha huyo mlemavu kupelekwa katika hospitali ya wagonjwa wa akili kwa uchunguzi.

Mwanariadha huyo mlemavu wa miguu yote miwili amekuwa akikanusha kumuua kwa makusudi mpenzi wake huyo Reeva Steenkamp.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni