Polisi mjini Limuru wakimwaga pombe haramu ya kienyeji. Watu 9 wamefariki dunia baada ya kunywa pombe ya kienyeji katika kijiji cha Kawamwaki, Limuru nchini Kenya.
Watu wengine 5 walipoteza maisha yao katika mazingira kama hayo jumanne katika kijiji cha Ikutha katika jimbo la Kitui.
Taarifa zaidi zinasema idadi ya vifo vilivyosababishwa na pombe hiyo Embu vimeongezeka na kufikia 18 huku watu wengine 40 wakiwa hospitali taabani wakipatiwa matibabu.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni