Rais wa Afrika Kusini Jackob Zuma
amesema wahalifu walivunja nyumba yake iliyopo kijijini zaidi ya
muongo mmoja uliopita na kumbaka mke wake, katika maelezo yake
aliyotoa kujitetea kutokana na matumizi makubwa ya dola milioni 23 ya
ukarabati wa nyumba hiyo ili kuboresha usalama.
Maelezo hayo ya rais Zuma ameyatoa
wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utakaofanyika Jumatano
wiki hii, ambapo ameongeza kuwa wahusika wa tukio hilo la kumbaka
mkewe wamekamatwa, kushtakiwa na kuhukumiwa baada ya kufanya uhalifu
huo kwenye nyumba yake iliyopo Nkandla KwaZulu-Natal kabla hajawa
rais mwaka 2009.
Hata hivyo rais Zuma hakuelezea ni mke
yupi aliyebakwa kati ya wake zake wanne ambapo mmoja wao alijiua, na
mwingine kutengana naye aitwaye Nkosazana Dlamini-Zuma ambaye kwa
sasa ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika.
Rais Zuma amekosolewa vikali kwa
matumizi makubwa ya fedha za walipa kodi, hata hivyo anatarajiwa
kushinda uchaguzi mkuu.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni