.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 14 Mei 2014

SAMIR NASI, CLICHY, KAKA, MOURA, TEVEZ NA LAMELA WAACHWA KWENYE VIKOSI VYA KOMBE LA DUNIA


Kiungo Samir Nasri ameachwa katika kikosi cha Ufaransa kitakachocheza Kombe la Dunia, ikiwa ni siku mbili tu kupita tangu aisadie timu yake ya Manchester City kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Mbali na Nasri, mchezaji mwenzake wa Manchester City Gael Clichy nae ameachwa nje ya kikosi cha taifa kinachonolewa na Didier Deschamps.

Wakati huo huo mshambulia wa Tottenham, Erik Lamela pamoja na mshambuliaji wa Juventus Carlos Tevez nao wamejikuta wakiachwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Argentina itakayocheza michuano ya Kombe la Dunia.

Nao uteuzi wa kikosi cha Brazili kitakachocheza michuano hiyo umeshuhudia kuachwa kwa wachezaji wawili wa AC Milan wenye majina makubwa ambao ni Kaka na Robinho, wakati Luiz Felipe Scolari akitangaza kikosi chake cha wachezaji 23, ambacho pia kimemuacha kiungo wa PSG Lucas Moura.
                                                                     Kaka na Robinho

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni