Beki Nemanja Vidic amekanusha tuhuma
kuwa wachezaji wa Manchester United waliacha kufanya jitihada wakati
wakinolewa na kocha David Moyes.
Katika mahojiano ya kina aliyofanya na
BBC, Vidic ameelezea namna wachezaji wa United walivyokuwa
wakikabiliwa na machungu katika chumba cha kubadilishia nguo kutokana
na matokeo mabaya, kiasi cha hata kulumbana kwa baadhi ya wachezaji.
Mchezaji huyo raia wa Serbia amekanusha
kuwa Manchester United ilifanya vibaya kutokana na kutomuheshimu
kocha David Moyes.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni