.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 7 Mei 2014

UBALOZI WA MAREKANI WATAHADHARISHA JUU YA MIPANGO YA KUSHAMBULIWA MAKANISA UGANDA

Ubalozi wa Marekani umesema makanisa nchini Uganda yapo katika hatari ya kukabiliwa na mashambulio ya kigaidi wakati huu ambopo Kenya ikikabiliwa na matukio ya mfulululizo ya milipuko ya mabomu inayofanywa na wapiganaji wa kundi la al Shabaab.

Taarifa ya Ubalozi wa Marekani iliyotolewa imesema wapiganaji wa kiislam wanapanga kufanya mashambulizi katika nyumba za Ibada Jijini Kampala kati ya mwezi huu ama mwezi Juni.

Taarifa hiyo haijaelezea kundi lolote linalopanga njama hizo ingawa kundi la Somalia la al Shabaab lenye uhusiano na al Qaeda limekuwa likilaumiwa kwa kuhusishwa na matukio kadhaa ya mashambulizi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni