Kuwa na misuguano na
mabishano ya mara kwa mara na mwenza wako, rafiki ama ndugu kunaweza
kuongeza nafasi ya mtu kuwa kwenye hatari ya kufa, hususani kwa wale
walio kwenye umri wa ujana.
Wataalam wa Denmark
wameeleza katika Jarida la Afya ya Jamii, kuwa wanaume wasio na kazi
ambao huwa muda mwingi nyumbani na wenza wao na kujikuta katika
misuguano na mabishano wapo katika hatari kufa.
Aidha, kukabiliana na hofu
na mahitaji ya familia pia kumehusishwa na idadi kubwa ya vifo vya
watu kwa mujibu wa utafiti huo.
Takwimu zinaonyesha
wanaume 9,875 na wanawake wenye umri kati ya miaka 36 and 52
waliojikuta katika mahusiano yaliyojaa msongo wanaishia kufariki
mapema.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni