Mwanamke mmoja raia wa Uingereza ambaye alikuwa amekunywa pombe, amehojiwa na polisi wa Marekani baada ya kuripotiwa kukamatwa akifanya mapenzi katika choo ndani ya ndege wakati akiwa safarini.
Wahudumu wa ndege hiyo ya Virgin Atlantic wamesema, mwanamke huyo anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 alikuwa safarini na wazazi wake, kabla ya kutoweka katika kiti chke na mwanamme mmoja waliyekuwa wamekaa naye, na baadaye kukamatwa wakifanya kitendo hicho katika choo cha ndege baada ya wahudumu wa ndege kuwalazimisha wafungue mlango.
Ndege hiyo ilikuwa inatokea London kuelekea Las Vegas Marekani mwishoni mwa wiki iliyopita, na baada ya kukabidhiwa kwa polisi alihojiwa na kuachiwa baada ya kupewa onyo na maofisa hao.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni