Rais Goodluck Jonathan amekiri kuwa
vikosi vya ulinzi vya Nigeria bado havijui walipo wasichana 230
waliotekwa nyara na kundi la Boko Haram.
Wasichana hao wanafunzi walitekwa wiki
tatu zilizopita kutoka kwenye shule yao huko Borno, na kundi la
wapiganaji wa Kiislam.
Rais Jonathan ametoa kauli hiyo kwa
mara ya kwanza tangu kutoweka kwa wanafunzi hao wasichana huku
serikali yake ikilaumiwa kwa kutochukulia kwa umakini sula hilo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni