.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 15 Mei 2014

WAKENYA WACHANGANYIKIWA BAADA YA DIVOCK ORIGI OKOTH KUAMUA KUCHEZEA UBELGIJI

                                                 Divock Origi Okoth wa kati kati 

Vyama vya soka, makocha na mashabiki wa mchezo huo nchini Kenya, wamepokea kwa hisia tofauti uamuzi wa mchezaji Divock Origi Okoth, kuamua kuchezea timu ya taifa ya Ubelgiji badala ya taifa lake la Kenya.

Wakati wadau wa soka wa Kenya wakiwa katika mkanyanyiko wa mawazo, mchezaji huyo ameelezea hisia zake na furaha aliyonayo ya kwa kupata nafasi ya kuliwakilisha taifa lake kwenye michuano ya kombe la dunia.

Divock mwenye umri wa miaka 19, ni mtoto wa aliyekuwa mchezaji wa kimataifa wa Kenya Mike Origi Okoth, ameitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ubelgiji cha wachezaji 24, na kuondoa nafasi ya kinda huyo kuiwakilicha nchi ya wazazi wake ya Kenya.

Mkuu wa Utawala wa Soka Kenya Robert Asembo amesema Kenya ilikuwa inamuhitaji Okoth kutokana na kuwa na kipaji cha soka cha aina yake lakini kutokana na uamuzi wake huo wanamtakia kila la kheri kama wanavyomtakia kila la kheri rais Barack Obama.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni