Waziri Mkuu wa zamani wa Israel, Ehud Olmert ( pichani ) aliyejiuzulu 2008, amehukumiwa kifungo cha miaka sita gerezani na mahakama moja nchini Israel baada ya kupatikana na makosa ya kupokea rushwa.
Olmert alipatikana na makosa mwezi Machi kwa madai ya kupokea rushwa ili kuharakisha ujenzi wa majengo ya kifahari katika mji mtakatifu wa Jerusalem.
Ehud Olmert alipatikana na makosa hayo wakati akiwa Meya wa Jerusalem. Alifanikiwa baadaye kuwa Waziri Mkuu wa Israel 2006 baada ya Ariel Sharon kuugua ugonjwa wa kiharusi.
Muonekano wa mji huo uliomuingiza matatizoni Olmert.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni