.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 13 Mei 2014

CHIFU APIGWA NA KUJERUHIWA NA WAUZA GONGO NCHINI KENYA

Chifu amejeruhiwa vibaya nchini Kenya baada ya watengenezaji pombe za kienyeji kuanzisha vurugu,kumpiga na kumjeruhi kwa kumkata na kitu chenye makali kwenye paji la uso na kwenye mkono.

Chifu Ezekiel Karanja wa eneo la Kasarani amelazwa katika kituo cha afya cha Elburgon, baada ya kushambuliwa na vijana kwa madai ya kuchochea wanakijiji kuvamia nyumba iliyohifadhi pombe haramu ya chang'aa (gongo) muda mfupi baada ya kuletwa.

Vijana hao walimvamia Chifu Karanja, ambaye alienda katika nyumba hiyo iliyotelekezwa akiwa peke yake.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni