Mwanariadha wa Uingereza aliyetwaa
medali mbili za mbio za Olimpiki Mo Fraha atashiriki mbio za mwaka
huu za michuano ya Jumuiya ya Madola zitakazofanyika huko Glasgow.
Farah, alishika nafasi ya nane katika
mbio za marathoni za London mwezi Aprili alikuwa hajaamua iwapo
atakimbia mbio za Glasgow.
Kocha wake Alberto Salazar, alimshauri
Farah kutokimbia tena hadi michuano ya Olimpiki ya Rio 2016.
Umamuzi huo wa Mo Farah umeongeza
matumaini kwa waandaji wa michuano hiyo, kutokana na mwanariadha
Muingereza Jessica Ennis-Hill kutoshiriki kutokana na kutarajia
kujifungua wakati Mjamaica Usain Bolt akiwa bado hajathibisha
kushiriki.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni