Wananchi wakiliangalia gari dogo aina ya Noah ambalo limeharibika upande wa kulia, baada ya kukwaruzwa na lori la kubeba mchanga maeneo ya Tegeta jijini Dar es Salaam leo mchana. Hakuna mtu aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa katika ajali hiyo
Askari wa usalama barabarani akichukua maelezo baada ya kutokea kwa ajali iliyohusisha lori la kubeba mchanga na gari dogo aina ya Noah maeneo ya Tegeta karibu na njia panda ya kuelekea kiwanda cha Wazo leo mchana. Picha hizi zimepigwa na msomaji wetu akiwa ndani ya gari wakati akipita eneo la tukio.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni