.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 3 Juni 2014

LUPITA NYONG'O APATA DILI LA KUIGIZA KWENYE FILAMU MPYA YA STAR WARS

Mshindi wa tuzo ya Oscar mwenye asili ya Kenya Lupita Nyong'o pamoja na nyota wa filamu ya Game Of Thrones, Gwendoline Christie ni miongoni mwa waigizaji wapya waliopata dili la kujiunga hivi karibuni katika upigaji picha ya filamu ya mpya ya Star Wars.

Lupita aliyetwaa tuzo hiyo kutokana na kushiriki vyema kwenye filamu ya 12 Years A Slave ataungana na nyota wengine kama John Boyega, Daisy Ridley, Adam Driver, Oscar Isaac, Andy Serkis, Domhnall Gleeson, na Max von Sydow katika filamu hiyo mpya itakayoongozwa na J.J. Abrams.

Katika kuonyesha furaha aliyonayo Lupita ameandika kwenye Instagram yake pamoja na kuweka picha ya Logo ya Star Wars, kuwa anaelekea kwenye galaxy mbali mbali kabisa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni