.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 13 Juni 2014

MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA TAMASHA LA VITABU VYA WATOTO MKOA WA DAR ES SALAAM


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akionyesha moja ya kijarida cha hadithi kwa ajili ya watoto alichokichagua kwa ajili ya kuwasomea hadithi watoto wakati akizindua rasmi Tamasha la vitabu vya watoto kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa hapa Dar Es Salaam tarehe 12.6.2014.

Mgeni Rasmi katika sherehe za uzinduzi wa Tamasha la vitabu kwa wanafunzi wa Shule za Msingi katika Mkoa wa Dar es Salaam, Mama Salma Kikwete akiongea na wanafunzi wakati wa uzinduzi huo kwenye ukumbi wa Makumbusho terehe 12.6.2014.


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkabidhi mtoto Edda Kasika kutoka Shule ya Msingi Maktaba tuzo kwa kushika nafasi ya pili katika uandishi wa insha katika Mkoa wa Dar es Salaam wakati wa uzinduzi rasmi wa tamasha la vitabu kwa watoto tarehe 12.6.2014.

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi washindi wa insha na mchapishaji wa vitabu bora vya watoto na wageni waalikwa mara baada ya kuzindua rasmi tamasha la vitabu vya watoto wa shule tarehe 12.6.2014.


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiangalia maonyesho ya vitabu, vijarida na kazi mbalimbali zilizokuwa zikionyeshwa na wanafunzi wa shule za msingi mkoani Dar es Salaam wakati wa sherehe za uzinduzi wa Tamasha la vitabu vya watoto tarehe 12.7.2014. 

                                                                          PICHA NA JOHN LUKUWI.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni