.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 13 Juni 2014

UPASUAJI WA MATOBO LAPAROSCOPIA WAFANYIKA LIVE KAIRUKI HOSPITALI

Daktari Bingwa wa upasuaji Dk. Muganyizi Kairuki akizungumza wakati wa semina ya upasuaji kwa njia matobo Laparoscopia uliofanyika LIVE katika Hospitali ya Kairuki Mikocheni jijini Dar es Salaam. Semina hiyo iliwashirikisha madakatari wa ndani na nje ya nchi. 

Daktari Bingwa wa upasuaji kutoka Afrka Kusini, Prof. Zacharia Koto (wa pili kulia), akisaidiana na daktari bingwa wa upasuaji kutoka Namibia Dk. S. Kaikai (kulia) na Dk. Muganyizi Kairuki wakimfanyia operesheni ya kuondoa mawe tumboni mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Kairuki, wakati wa semina ya upasuaji kwa njia ya matobo iliyofanyika katika hospitali ya Kairuki Mikocheni jijini Dar es Salaam.

                                      Madaktari wakishauriana jambo wakati wa operesheni.
Kutoka kushoto ni Dk. Ali Mwanga wa Muhimbili, Dk. Steven Mbata wa Kairuki Hospitali, Dk. Brown Ndofor wa Namibia Dk. Sunil Popat wa India na Sister Salvata Kulaya wa Kairuki Hospitali.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni