.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 12 Juni 2014

NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUWASILISHA BAJETI ZAO ZA 2014/2015 LEO

                                                   Waziri wa Fedha wa Tanzania Saada Mkuya 
 
Nchi za Afrika Mashariki leo zinawakilisha bajeti zao za serikali kwa mwaka 2014-2015 katika mabunge yao, chini ya utaratimu waliojiweka wa kuwakilisha bajeti hizo katika siku moja.

Nchini Tanzania Waziri wa Fedha wa Tanzania, Saada Mkuya atawasilisha bajeti ya trilioni 19.6 katika bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.

Nchini Kenya Waziri wa Fedha wa Nchi hiyo Henry Rotich atawasilisha bungeni Jijini Nairobi bajeti ya mwaka 2014/2015 ya shilingi trilioni 1.8 za Kenya ikiwa ni bajeti kubwa katika historia ya nchi hiyo.

Huko Uganda Waziri wa Fedha Maria Kiwanuka naye hii leo atawasilisha bajeti ya serikali ya mwaka 2014/2015 ya shilingi trilioni 14 za Uganda katika bunge la nchi hiyo huku kipaumbele kikiwa ni miundombinu.
                                                          Waziri wa Fedha wa Kenya Henry Rotich
                                             Waziri wa Fedha wa Uganda Maria Kiwanuka

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni