.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 12 Juni 2014

UZINDUZI WA KAMPENI KUCHANGIA DAMU


Diwani Bonna Kaluwa akitoa takwimu za vifo vinavyotokana na ukosefu wa damu wakati wa uzinduzi wa kampeni yake ya kuchangisha damu salama ili kuokoa vifo hivyo. Kampeni hiyo imezinduliwa Dar es Salaam leo na kilele chake ni Juni 22, mwaka huu. Diwani huyo wa Kipawa pia amewahamasisha Watanzania kujitokeza kuchangia damu salama. ( Picha zote na Oscar Mbuza)

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakifuatilia uzinduzi wa kampeni ya uchangishaji wa damu iliyozinduliwa Dar es Salaam leo na Diwani wa Kata ya Kipawa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bonna Kaluwa.

Afisa Viwango na Ubora wa Damu Salama Kanda ya Mashariki, Ndeonasia Towo akizungumza leo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuchangia damu salama inayoratibiwa na Diwani wa Chama cha Mapinduzi wa Kata ya Kipawa, Bonna Kaluwa (katikati) iliyozinduliwa katika Ukumbi wa Arnaotoglu na kilele chake kitakuwa Juni 22, mwaka huu kwenye viwanja vya Sitakishari Kata ya Kipawa, Dar es Salaam. Kampeni hiyo inalengo la kuchangisha damu ili kupunguza vifo vya wanawake wakati wa kujifungua kutokana na ukosefu wa damu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni