.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 12 Juni 2014

KOMBE LA DUNIA KUGONGANA NA MFUNGO WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

                      Wachezaji wa Ivory Coast ndugu Yaya na Kolo Toure ni Waislam
 
Baadhi ya nyota wa Kombe la Dunia ambao ni waumini wa dini ya Kiislam watajikuta katika wakati mgumu kutoathiri ufanisi wao dimbani na kuweza kutimiza imani yao ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan unaotarajiwa kuanza wakati michezo hiyo ikiendelea.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 1986 kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan kugongana na michuano ya Kombe la Dunia.

Waumini wa Dini ya Kiislam huwa wanafunga kuanzia alfajiri hadi Jioni ambapo huwa hawali chakula chochote kwa muda huo wala kinywaji, jambo ambalo litaathiri ufanisi wa wachezaji kadhaa wa imani hiyo huko Brazil. 

                                 Mchezaji wa Ufaransa Karim Benzema naye ni Muislam
                    Mshambuliaji wa Switzerland Xherdan Shaqiri naye ni Muislam


 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni