.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 31 Julai 2014

BARAZA LA WAWAKILISHI MAREKANI LATAKA KUMFUNGULIA MASHTAKA RAIS OBAMA


Baraza la Wawakilishi la Marekani limepitisha azimio la kumshtaki Rais Barack Obama kwa madai ya kuenda kinyume na mamlaka yake ya Kikatiba.

Kura 225 dhidi ya 201 zilizopigwa kwa misingi ya kisiasa zinatoa fursa kwa mawakili wa baraza hilo kuandaa nakala za kisheria kwa ajili ya kufungua kesi hiyo.

Wanaounga mkono azimio hilo wanasema Rais Obama alivuka madaraka yake wakati alipochelewesha muda wa kikomo wa bima katika mpango wa sheria ya afya.

Hata hivyo Rais Obama amepuuzia mpango huo wa kumshtaki kwa kusema ni upotevu wa muda, na kuongeza kuwa kila mtu anaonajuhudi hizo ni za kutafuta umaarufu wa kisiasa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni