.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 29 Julai 2014

COASTAL UNION KUKIPIGA NA AFRICAN SPORTS KESHO MKWAKWANI

TIMU ya Coastal Union ya Tanga "Wagosi wa Kaya" kesho inatarajiwa kucheza mechi ya kirafiki na African Sports “Wanakimanumanu”kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani itakayokuwa ya kusheherekea sikukuu ya iddi Pili.

Akizungumza leo Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga amesema maandalizi ya kuelekea mchezo huo yamekamilika kwa asilimia kubwa na kinachosubiriwa na mechi hiyo itakayoanza saa kumi jioni kwenye uwanja huo.

El Siagi amesema baada ya kumaliza mechi hiyo timu hiyo itaelekeza mipango yake ya kucheza mechi za kirafiki nyengine ili kuweza kujiweka imara kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara.

Amesema wachezaji wa timu hiyo wataingia kwenye mechi hiyo kwa malengo ya kupata ushindi ili kuweza kuendeleza rekodi ya kuwafunga wanakumanumanu hao ambao msimu ujao watashiriki michuano ya ligi daraja la kwanza.

Kwa upande wake,Ofisa Habari wa timu ya African Sports,Wanakimanumanu”Said Karsandas amesema kuwa wamepania kushinda kwenye mechi hiyo ili kuweza kurudisha ile heshima ya timu hiyo kwa wagosi hao wa kaya.


Tunajua mechi hii itakuwa ni ngumu kutokana na uwezo wa Coastal Union hivyo nasi tumejipanga kuweza kufanya vizuri ili kutoa burudani kabambe “Alisema Karsandas.

Hata hivyo aliwataka wakazi wa mkoa wa Tanga na viunga vyake kujitokeza kwa wingi kushuhudia burudani itakayokuwa ikitolewa kwenye mechi hiyo .

Oscar Assenga .
Msemaji wa Coastal Union.
0714453839,Tanga.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni