.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 29 Julai 2014

WANAKIJIJI WAKAMATA LORI LILILOKUWA NA NGUZO ZA UMEME ZILIZOIBIWA


Na: Shushu Joel
Wana kijiji wa kijiji cha jijabirishi wilayani maswa mkoani simiyu wamelikamata gari aina ya center lenye namba za usajili T 591 AFJ mali ya BASEMA lenye makazi yake jijini mwanza.

Gari hilo lilikamatwa majira ya saa moja jioni likiwa na nguzo za umeme 16 katika maeneo ya nyambiti mpakani mwa wilaya ya magu na maswa zikiwa zinapelekwa mkoani mwanza kwa ajili ya biashara.
Nguzo hizo ni mali ya kampuni ya Sengerema Engineening Group Limited inayosambaza umeme katika vijiji mbalimbali mkoani simiyu kwa kupitia mradi wa umeme vijijini ambao unasimamiwa na serikali ya Jamhuli ya Muungano wa Tanzania.

Dereva wa gari hilo alinusurika kifo toka kwa wananchi hao kwa msaada wa polisi wa kituo kidogo cha nyambiti ambao waliwahi kufika katika tukio hilo na kuwaomba wananchi wasifanye chochote kwani huyu dereva alikuwa ajui kinachoendelea juu ya tukio hili kwa sababu yeye kaagizwa na boss wake ambaye ni Bw, BASEMA kuja kuchukua mzigo huo wa nguzo za umeme.


Akizungumza mara baada ya kuokolewa na polisi dereva wa gari hili aliyejitambulisha kwa jina la Daniel Peter mwenye umri wa miaka 29 amesema kuwa yeye ufanya shughuli za ubebaji wa mizigo mbalimbali na gari lake hivyo alipigiwa simu na boss na kisha kuambiwa aweke mafuta ya laki moja kwani kuna safari ya kilometa nyingi kidogo na kisha kufanya kama alivyoagizwa na boss wake na ndipo alipoongozana na wenyeji wake wenye gari aina ya ....... Lenye namba za usajili T.........ambalo lilikimbia mara baada ya timbili hilo la wananchi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii msimamizi wa mradi huu wa umeme vijiji toka katika kampuni ya sengerema Engineening Group limited Bw, Juma musime amesema kuwa wakiwa katika kazi zao za usambazaji wa nyaya toka sehemu moja kwenda sehemu nyingine mara

anapigiwa simu na mwanakijiji wa jijabirishi na kumuuliza kuwa mbona hizi nguzo zinapelekwa mwanza au zimebaki? Ndipo hapo msimamizi huyo alipoomba msaada wake kwa kuwataarifu wanakijiji wenzake na kuanza kuzifuatilia nguzo hizo na kufanikiwa kuzikamata.

Bw, Juma aliongeza kuwa ukaribu wake na wananchi hao ndio nguzo ya mafanikio ya umeme katika mkoa huo na pia kulipongeza jeshi la polisi kwa msaada wao wa dhati na hata kuahidi kushilikiana nao katika mambo mbalimbali yenye tija katika taifa langu.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa simiyu, kamanda Charles Mkumbo amesema kuwa ni kweli tukio hilo limetokea na mpaka sasa dereva wa gari hilo anashikiliwa na polisi
kwa uchunguzi wa kisheria na mda si mrefu kesi hiyo itapandishwa mahakamani.

Kamanda mkumbo aliongeza kuwa anasikitishwa sana na watu wa aina hii kwani hawa ni wapinga maendeleo ya taifa kabisa lakini sheria itachukua mkondo wake na hata kuwa fundisho kwa watu wa namna hii.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni