.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 29 Julai 2014

TIMU YA TAIFA YA MCHEZO WA CHESS YAKABIDHIWA BENDERA YA TAIFA KWENDA KUSHIRIKI MASHINDANO YA KIMATAIFA NCHINI NORWAY


Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (katikati), akizungumza na wanahabri kabla ya kukabidhi bendera. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini na kulia mchezaji Hemed Mlawa.


Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini, akizungumza na wanahabari. Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi.


Wachezaji wa mchezo huo, Hemed Mlawa (kulia) na Emmanuel Mwaisumbe wakiwa kwenye hafla hiyo ya kukabidhiwa bendera ya Taifa. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Tanzania, Henry Lihaya.


Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (kulia), akimakabidhi Bendera ya Taifa, mmoja wa wachezaji wa timu ya Taifa wa mchezo wa Chess, Hemed Mlawa (wa pili kushoto), Dar es Salaam leo asubuhi kwa ajili ya kuondoka kesho kwenda kushiriki mashindano ya kimataifa nchini Norway. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini, kushoto ni mchezaji Emmanuel Mwaisumbe. Safari hiyo imedhaminiwa na Tanzania Chess Foundation na Kasparov Foundation.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni