Israeli imesema itachunguza kitendo
cha kutupa kombora kwenye shule inayokaliwa na raia waliokimbia
mapigano huko Gaza, na itaomba radhi iwapo ilihusika na kitendo
hicho.
Msemaji wa serikali ameviambia
vyombo vya habari, kuwa Israeli inasera ya kutowashambulia raia.
Marekani na Umoja wa Mataifa
wameshutumu shambulio hilo lililouwa watu 16, wakati mapigano hayo
yanayoendelea yakisababisha vifo vya watu 100 siku ya jumatano.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni