Mashiriki mengi ya ndege barani Ulaya yamesitisha safari zake kuelekea nchini Israel kufuatia mapigano yanayoendelea kati ya taifa hilo na kundi la Hamas lililopo katika ukanda wa Gaza.
Shirika la ndege la Delta, Shirika la ndege la Marekani na mashirika mengine ya ndege ya Ulaya yametangaza kusimamisha safari zake zote kuelekea katika uwanja wa ndege wa Ben Gurion ulipo mjini Tel Aviv.
Hapo jana jumanne ndege ya Delta namba 468 Boeing 747 iliyokuwa inatoka New York kuelekea Tel Aviv ikiwa na abiria 273 na wahudumu 17 wa ndege ililazimika kukatisha ruti hiyo na kuelekea Paris, Ufaransa kufuatia taarifa kuwa hali si shwari mjini Tel Aviv.
Taarifa za mashirika hayo kusitisha safari zake zimekuja baada ya kuripotiwa kuwa, makombora ya Hamas yameshambulia na kuharibu nyumba moja jirani na uwanja huo wa ndege wa Ben Gurion mjini Tel Aviv.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni