Makubaliano ya kusitisha mapigano kwa saa 12 kati ya Israel na kundi la Hamas yanaendelea kutekelezwa katika ukanda wa Gaza.
Raia wa palestina katika ukanda wa Gaza wameanza kurejea katika makazi yao yaliyoharibiwa vibaya na makombora ya Israel, baada ya hapo awali Israel kuwataka wakazi hao kuondoka katika makazi yao ili kuepuka mashambulizi na madhara zaidi juu yao.
Hata hivyo Israel imesema itaendeleza mashambulizi yake katika maeneo waliyopo wapiganaji wa Hamas
Raia wa Palestina wakirejea katika makazi yao baada ya kuwepo makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na kikundi cha Hamas
Mtoto akiwa na mito aliyoiokota katika mabaki ya makazi yao yaliyoharibiwa vibaya na makombora ya Hamas.
Uharibifu mkubwa uliofanywa katika makazi ya Wapalestina na majeshi ya Israel
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni