.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 30 Julai 2014

MAREKANI YATANGAZA VIKWAZO DHIDI YA URUSI

 Marekani imeendelea kuiwekea vikwazo zaidi Urusi, hii ni kufuatia mgogoro unaoendelea nchini Ukraine ambapo Urusi inawaungwa mkono waasi wanaoipinga serikali iliyopo madarakani.

Akihutubia usiku wa kuamkia leo akiwa ikulu ya Marekani White House, Rais Barack Obama amesema kuwa vikwazo hivyo ni katika sekta za Nishati, Silaha na Fedha. 

Katika hotuba yake hiyo, Obama amesema vikwazo hivyo kwa Urusi haviwezi kuanzisha vita baridi. 

Aidha ameitaka Urusi kuacha kuwaunga mkono waasi na kuyaondoa majeshi yake katika mpaka wa Ukraine, huku pia akisisitiza Urusi ifanye juhudi za kuhakikisha waasi wanarejea katika meza ya mazungumzo ili kumaliza machafuko.
                                                                                    Rais wa Urusi, Vladmir Putin

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni