KILO 260 ZA MENO YA TEMBO ZAKAMATWA KATIKA UWANJA WA KIMATAIFA WA JOMO KENYATTA LEO
Maafisa wa Mapato Kenya leo
wamekamata kilo 260 za meno ya tembo kwenye jengo la mizigo la
Swissport katika uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta Jijini Nairobi.
Mamlaka ya Mapato Kenya (KRA)
imesema meno hayo yalikuwa yasafirishwe kimagendo kwenda Kuala
Lumpur, Malaysia kwa kutumia nyaraka feki.
Meno hayo ya tembo yanakadiriwa kuwa
na thamani ya shilingi milioni 39 za Kenya.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni