.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 25 Julai 2014

MAGAVANA NCHINI KENYA WAKOSA FEDHA ZA MISHAHARA YA WATUMISHI WA KAUNTI

                          Mdhibiti wa Bajeti wa Serikali ya Kenya Agnes Odhiambo

Magavana nchini Kenya watahadharisha kuwa utendaji wa kaunti zao utasimama kutoka na wabunge kuchelewesha kupitisha sheria itakayoridhia kutolewa shilingi bilioni 226.6 za Kenya kwa ajili ya kuendesha serikali za kaunti.

Wakiongea katika mkutano na waandishi wa habari magavana wamesema kaunti zitashindwa kulipa mishahara ya mwezi huu kwa ajili ya huduma za afya kutokana na kutokuwepo kwa fedha kwenye akaunti za kaunti.

Kufuatia kilio hicho cha magavana mdhibiti wa bajeti ya serikali Agnes Odhiambo ameagiza kutolewa kwa nusu ya fedha hizo baada ya kufikiwa makubaliano mahakamani baina ya mabaraza ya kaunti na mamlaka ya mapato Kenya (KRA).

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni