Mama wa watoto wawili nchini
Uingereza ameelezea mateso aliyopitia kwa miaka miwili baada ya
vipimo kuonyesha kimakosa anaugua saratani mbaya ambapo madaktari
walimuambia ataishi kwa muda wa miaka miwili tu.
Mama huyo Denise Clark, ilibidi
aandae mipango ya mazishi yake, na kuandika ujumbe wenye kuvuta hisia
wa kuwaaga watoto wake wawili ambao mmoja ni mwanaume na mmoja
mwanamke..
Hata hivyo Clark aliamua kwenda
Hispania kupatiwa tiba mbadala ili kuongeza muda wa kuishi, na baadae
baada ya kufanyiwa vipimo madaktari walibaini kile walichodhani kuwa
ni saratani ni kovu lililobakia zamani wakati akitibiwa saratani
katika miaka ya nyuma.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni