Mwanamke mmoja aitwae Saudatu Koroma
raia wa Sierra Leone aliyetoroka hospitali baada ya kubainika kuwa na
virusi vya ugonjwa hatari wa Ebola, amefariki dunia baada ya
kujisalimisha tena hospitali.
Familia ya mwanamke huyo
ilimlazimisha kutoka hospitali ya umma siku ya Alhamis, akiwa ni
mgonjwa wa kwanza kuripotiwa katika Jiji la Freetown, ambako hakuna
chumba maalum kwa wagonjwa wa Ebola.
Tangu mwezi Februari mwaka huu zaidi
ya watu 660 wamekufa kwa ugonjwa wa Ebola Afrika Magharibi, ikiwa ni
mlipuko hatari kuliko wote wa ugonjwa huo kutokea duniani.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni