Rais Uhuru Kenyatta leo amewaambia
viongozi wa upinzani nchini Kenya kuachana na masula ya kutoa lugha
chafu na badala yake wajihusishe na siasa zenye kujenga nchi.
Amesema viongozi wa CORD
wanaoongozwa na Raila Odinga wanapaswa kurejea kwenye siasa za
kiutuuzima na kuachana na tabia ya kutoa mara kwa mara vitisho na
lugha chafu kwa serikali iliyochaguliwa na wakenya wengi.
Rais Kenyatta amenukuliwa akisema
“anamtaka kaka Raila kuheshimu cheo cha urais, kwani iwapo ingekuwa
ni yeye Raila kachaguliwa kuwa rais, Kenyatta asingeweza kusimama
barabarani na kumtukana”.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni