.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 27 Julai 2014

MWENGE WA UHURU WAWASILI MKOA WA DAR ES SALAAM

IMG_5968
Mkuu wa Wilaya ya Mafia Sauda Salum Mtondoo akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara Hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana James Kajugusi alipowasili wakati wa kuukabidhi mwenye wa uhuru kutoka wilaya yake.IMG_5976
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akisalimiana na Vijana wakimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa walipowasili kutoka Wilaya ya Mafia  IMG_5994
Mkuu wa Wilaya ya Mafia Sauda Salum Mtondoo akikimbiza Mwenge wa Uhuru kwa ajili ya kuukabidhi tayari kuanza ziara yake Mkoani Dar es Salaam. IMG_6017
Mkuu wa Wilaya ya Mafia Sauda Salum Mtondoo (Mwenye T-shirt nyeupe) akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza Leo Jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza akikimbiza mwenge wa Uhuru Tayari kwa kuukabidhi kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki.
IMG_6040
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akisalimiana na Kiongozi wa mbio za Mwenge Taifa, Rachel Kasanda wakati wa kuwasili kwa mwenge wa uhuru leo Jijini Dar es Salaam. IMG_6043
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki leo Jijini Dar es Salaam. IMG_6058Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akitoa neno la shukrani kwa Mkuu wa Pwani Bi. Mwantumu Mahiza kwa Kuukabidhi mwenge wa Uhuru Salama Mkoani Dar es Salaam. IMG_6064
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akishika mwenge wa Uhuru ulipowasili mkoani Dar es Salaam.IMG_6065
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akishika mwenge wa Uhuru ulipowasili mkoani Dar es Salaam.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni