Mkurugenzi wa Shirika la Ndege la
Malaysia,Bw. Hugh Dunleavy akiongea na waandishi wa habari.
Shirika la Ndege la Malaysia
linajipanga kufanya mabadiliko makubwa kufuatia matukio makuu mawili
ya majanga yaliyolikumba shirika hilo ndani ya miezi sita.
Shirika hilo limesema linaangaliwa
uwezekano wa kufanya mambo kadhaa katika kujiimarisha kibiashara
ikiwemo kubadili jina la shirika hilo.
Katika mabadiliko hayo pia shirika
hilo linafikiria kuanzisha safari katika njia mpya, na kuongeza
ushirika na wadau wa usafiri huo ili kupata faida.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni