Mipaka yote inayoingia Liberia
imefungwa na jamii iliyokumbwa na ugonjwa wa Ebola wanakabiliwa na
zuio la kutotoka maeneo yao katika kujaribu kuzuia kusambaa kwa
virusi vya ugonjwa huo.
Vituo vya vya kupima ugonjwa huo
vimewekwa katika maeneo makuu machache yanayoruhusiwa kuingia, kama
vile uwanja wa ndege.
Wakati huo huo shirika kubwa la
ndege la Nigeria la Arik Air, limesitisha usafiri wa ndege zake
kwenda Liberia na Sierra Leone baada ya mtu aliyeugua Ebola kuingia
kwa ndege Nigeria wiki iliyopita.
Ugonjwa wa Ebola umeuwa watu 660
katika nchi za Afrika ya Magharibi tangu Februari.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni