Waziri Mkuu wa Israeli ametoa onyo
la kuendeleza mapigano huko Gaza, ambapo jana usiku mabomu mengi
yametupwa tangu mapigano hayo yaanze.
Waziri Benjamin Netanyahu amesema
Israeli itaendelea kushambulia Gaza hadi hapo ifikie malengo yake ya
kuuteketeza mtandao wa aridhini wa Hamas.
Israeli imefanya mashambulizi ya
anga kwa kutupa mabomu 60 huko Gaza usiku na kushambulia kituo cha
televisheni cha Al-Aqsa na Redio ya Al-Aqsa pamoja na nyumba ya
kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh.
Kiongozi wa Hamas, Ismail Haniyeh
ambaye nyumba yake imeshambuliwa kwa mabomu.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni